KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Tuesday, December 16, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan afungua Mkutano wa 9 wa CDF na Makamanda




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga kwa ajili ya kufungua mkutano wa 9 wa CDF na Makamanda tarehe 15 Desemba 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wakuu wa Kamandi, Wakuu wa Matawi na Makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kabla ya kufungua mkutano wa 9 wa CDF na Makamanda uliofanyika katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga tarehe 15 Desemba 2025.

Matukio mbalimbali wakati wa mkutano wa 9 wa CDF na Makamanda uliofanyika katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga. Mkutano huo wa CDF na Makamanda ulifunguliwa na rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 15 Desemba 2025.

Monday, December 15, 2025

WAZIRI MKUU: WATANZANIA TUNZENI AKIBA YA CHAKULA

*Ahimiza matumizi ya mbolea na mbegu za mazao ya muda mfupi


WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania watunze akiba ya chakula walichonacho na waepuke matumizi yasiyofaa kutokana na hali ya kuchelewa kwa msimu wa mvua.


Waziri Mkuu ametoa wito huo leo jioni (Jumapili, Desemba 14, 2025) wakati akizungumza na baadhi ya Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya, ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma.


Amewaeleza viongozi hao kutoka mikoa ya Dodoma na Singida kwamba Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilitoa utabiri wa mwelekeo wa msimu wa mvua za vuli na mvua za msimu kwa kipindi cha Oktoba 2025 hadi Desemba 2025 na kipindi cha mwezi Novemba, 2025 hadi Aprili 2026 mtawalia. 


“Kutokana na utabiri huo, baadhi ya mikoa nchini inatarajiwa kuwa na mvua za chini ya wastani hadi wastani na kutawaliwa na vipindi virefu vya ukavu na mtawanyiko wa mvua usioridhisha,” amesema. 


Amesema tathmini hiyo ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inaonesha hali ya kuchelewa kwa mvua inatarajiwa katika maeneo ya mikoa ya Dodoma, Katavi, Kigoma, Singida, Tabora, Iringa, Mbeya, Mtwara, Njombe, Songwe, Rukwa, Ruvuma pamoja na Kusini mwa Mkoa wa Morogoro.


“Pamoja na kuwa hakuna tishio la uhaba wa chakula kutokana na hifadhi ya chakula iliyopo nchini, lakini ni vema, wananchi waendelee kuzingatia matumizi sahihi ya chakula. Tuna akiba ya chakula ya kutosha lakini ninawasihi wananchi waweke akiba na kuepuka matumizi yasiyo ya lazima,” amesema.


Ametumia fursa hiyo kuwakumbusha wakulima waandae mashamba kwa wakati na watumie pembejeo zinazoendana na upatikanaji wa mvua chache sambamba na kuzingatia ushauri wa wataalamu wa kilimo ambao kwa sasa wanazunguka nchi nzima kukutana na wakulima na kutoa elimu. 


Vilevile, Dkt. Mwigulu amewataka wafugaji wote waweke mipango mizuri ya matumizi na uhifadhi wa maji na vyakula vya mifugo ili kukabiliana na hali hiyo.


Waziri Mkuu amewasisitiza Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wahakikishe maafisa ugani wanawatembelea wakulima na kutoa ushauri ikiwemo matumizi sahihi ya mbegu kulingana na hali ya hewa badala ya kukaa ofisini muda wote.

“Vilevile, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri endeleeni kuhamasisha wakulima wajisajili kwenye daftari la mkulima na kuhakikisha wanapata namba za usajili,” amesisitiza.


Amewataka viongozi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) zihakikishe kuwa shehena za pembejeo zinahudumiwa kwa wakati ili usambazaji ufanyike kwa ufanisi.


RAIS DKT. SAMIA AONGOZA WAOMBELEZAJI KUAGA MWILI WA JENISTA MHAGAMA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza waombelezaji kuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho Marehemu Jenista Joakim Mhagama katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kiwanja Cha Ndege, Jimbo Kuu Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na waombelezaji mara baada ya ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho Marehemu Jenista Joakim Mhagama katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kiwanja Cha Ndege, Jimbo Kuu Dodoma.

Picha za matukio mbalimbali wakati wa ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho Marehemu Jenista Joakim Mhagama katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kiwanja Cha Ndege, Jimbo Kuu Dodoma.




MAKAMU WA RAIS KUWEKA JIWE LA MSINGI KAMPASI YA UDSM, KAGERA LEO


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Bukoba mkoani Kagera leo tarehe 14 Desemba 2025. Makamu wa Rais anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa Kampasi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mkoa wa Kagera, itakayofanyika tarehe 15 Desemba 2025.





 

Saturday, September 23, 2023

p style="text-align: center;">&nbsp;<span style="font-family: &quot;Times New Roman&quot;, &quot;serif&quot;; font-size: 18pt; text-align: center;">NA
K-VIS BLOG, GEITA.</span></p>

<p align="center" class="MsoNormal" style="text-align: center;"><span style="font-family: &quot;Times New Roman&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 18pt; line-height: 115%;">WANACHAMA
wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) wametakiwa kutumia
fursa ya Maonesho ya 6 ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya
Bombambili vilivyopo eneo la EPZA, mkoani
humo Geita, kufika kwenye banda la Mfuko huo ili kuhudumiwa na kupata elimu
inayohusiana na uanachama wao, <span style="mso-spacerun: yes;">&nbsp;</span>Meneja wa
PSSSF Kanda ya Ziwa Magharibi, Bw. <span style="mso-spacerun: yes;">&nbsp;</span>Geofrey
Kolongo, amesema.<o:p></o:p></span></p>

<p align="center" class="MsoNormal" style="text-align: center;"><span style="font-family: &quot;Times New Roman&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 18pt; line-height: 115%;">Ameyasema
hayo leo Septemba 22, 2023 kwenye banda la PSSSF, kwenye maonesho hayo ambayo PSSSF
ni miongoni mwa taasisi za umma zinazoshiriki ili kuwahudumia wananchi na
watumishi wanaoshiriki katika maonesho hayo.<o:p></o:p></span></p>

<p align="center" class="MsoNormal" style="text-align: center;"><i style="mso-bidi-font-style: normal;"><span style="font-family: &quot;Times New Roman&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 18pt; line-height: 115%;">“Tunatoa
huduma zote ambazo zinapatikana kwenye ofisi zetu zilizoenea kote nchini, ambambo
mwanachama ataweza kupata taarifa za Michango yake, taarifaz a Mafao yatolewayo
na PSSSF, Wastaafu wataweza kujihakiki kwa njia ya biometric, lakini pia elimu
kuhusu Hifadhi ya Jamii, jinsi ya kutumia huudma za PSSSF kiganjani, na taarifa
za uwekezaji.” Alisema Bw. Kolongo.<o:p></o:p></span></i>

</p>

<p align="center" class="MsoNormal" style="text-align: center;"><span style="font-family: &quot;Times New Roman&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 18pt; line-height: 115%;">Maonyesho
hayo ambayo hufanyika kila mwaka, yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi Septemba 23,
2023 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dotto Biteko na yatafikia
kilele Septemba 30, 2023.<o:p></o:p></span></p>

<p align="center" class="MsoNormal" style="text-align: center;"><span style="background: white; color: black; font-family: &quot;Times New Roman&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 18pt; line-height: 115%;">Maonesho hayo yenye kauli mbiu; Matumizi ya
teknolojia sahihi katika kuinua wachimbaji wadogo kiuchumi na kuhifadhi
mazingira yamewaleta pamoja washiriki zaidi ya 400.</span></p><p align="center" class="MsoNormal" style="text-align: center;"></p><div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEheqd2QHfoWbCazrPQw-O-Cl-zzLgzuNer3jHe87H8lBAZJ3_uHqeTj4ceN_YVGmNaic3XEMAbgsN4m_DzYGMT7E9V7TPxowJLmN-SoAOGWlNji4Q_1htfcu3YqfXZObZT7AdU5z283wySlGzg-UFmSAiORdmYPqLaZHqoxvBM8QYr3gWRS4spEOJj76t4/s6720/GL7A0081.JPG" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" data-original-height="4480" data-original-width="6720" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEheqd2QHfoWbCazrPQw-O-Cl-zzLgzuNer3jHe87H8lBAZJ3_uHqeTj4ceN_YVGmNaic3XEMAbgsN4m_DzYGMT7E9V7TPxowJLmN-SoAOGWlNji4Q_1htfcu3YqfXZObZT7AdU5z283wySlGzg-UFmSAiORdmYPqLaZHqoxvBM8QYr3gWRS4spEOJj76t4/s16000/GL7A0081.JPG" /></a></div><br /><div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgwyFj2Jaz8VGz2ACGnEd4hVhWcGLMtZlwM0xXR5MZVbH04xoPOoFRFKkJShlMii5ocXWu-3Yxba16y2Mp7pXvJn4MKVyko15c1THckdAnSKqwlW919gRsRZBIi58yKE45b_cjyvEtmxe59tArLPHf1VPyt2szMcxy7Hf6sF_MZBXMuTR2UJyzK126roIE/s6720/GL7A0011.JPG" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" data-original-height="4480" data-original-width="6720" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgwyFj2Jaz8VGz2ACGnEd4hVhWcGLMtZlwM0xXR5MZVbH04xoPOoFRFKkJShlMii5ocXWu-3Yxba16y2Mp7pXvJn4MKVyko15c1THckdAnSKqwlW919gRsRZBIi58yKE45b_cjyvEtmxe59tArLPHf1VPyt2szMcxy7Hf6sF_MZBXMuTR2UJyzK126roIE/s16000/GL7A0011.JPG" /></a></div><br /><div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhMXsuaAOBI-sl4gRy62l8yC5XcnZPZpnGa7CGN9gWAGJ4K9idcvEW5Y0aDiL6Y4TXGGDIXfBbaD4Wf_18yA_nYtIBq0S1qQCqGgkb2CsPIznpd8TwJbzXAKPVhFKLLRn28AfG4XTB9XXvKxoScbWQ36Y6wDQdvX--6PTbkyzKGBZnbgOPuqi2HDvVrIC0/s6720/GL7A0040.JPG" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" data-original-height="4480" data-original-width="6720" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhMXsuaAOBI-sl4gRy62l8yC5XcnZPZpnGa7CGN9gWAGJ4K9idcvEW5Y0aDiL6Y4TXGGDIXfBbaD4Wf_18yA_nYtIBq0S1qQCqGgkb2CsPIznpd8TwJbzXAKPVhFKLLRn28AfG4XTB9XXvKxoScbWQ36Y6wDQdvX--6PTbkyzKGBZnbgOPuqi2HDvVrIC0/s16000/GL7A0040.JPG" /></a></div><br /><div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi4MOcPpcDjlmipJewzQfB198YldFwW2dfUPnyMIHSK30A7vPCTyes_6ddFR7PyKfL_bdzOaxBYDALM1dni1WAwn7Y8W2pPD_sHIZ8F8PMLA8mHdWdbQN6eUDjRbRn7FUzQzihGViE7Ce93t5xxAu0J2J3vQhJUHGGjLyaTx3z8pfyjJA1M3PWZ-7Q4nJk/s6720/GL7A0108.JPG" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" data-original-height="4480" data-original-width="6720" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi4MOcPpcDjlmipJewzQfB198YldFwW2dfUPnyMIHSK30A7vPCTyes_6ddFR7PyKfL_bdzOaxBYDALM1dni1WAwn7Y8W2pPD_sHIZ8F8PMLA8mHdWdbQN6eUDjRbRn7FUzQzihGViE7Ce93t5xxAu0J2J3vQhJUHGGjLyaTx3z8pfyjJA1M3PWZ-7Q4nJk/s16000/GL7A0108.JPG" /></a></div><br /><div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjkG9WcUPL01Dku0BVl1T1Mvs0XoCBDVYqnZVpkHgExt-uuI9BdSNXsHtDam-rTWkpMz1zb3idu-RIiaQT00dAPaDDcmsfF2LVoyQ10Po6Ll05QyhZasZAEZvJf2Tqrjj_h0748t0ZZzCStx9lne6X7SwfmOxEcM_7ihV3Av5JjtPlDJtdrkXf1GqdfUyY/s6720/GL7A0053.JPG" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" data-original-height="4480" data-original-width="6720" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjkG9WcUPL01Dku0BVl1T1Mvs0XoCBDVYqnZVpkHgExt-uuI9BdSNXsHtDam-rTWkpMz1zb3idu-RIiaQT00dAPaDDcmsfF2LVoyQ10Po6Ll05QyhZasZAEZvJf2Tqrjj_h0748t0ZZzCStx9lne6X7SwfmOxEcM_7ihV3Av5JjtPlDJtdrkXf1GqdfUyY/s16000/GL7A0053.JPG" /></a></div><br /><span style="background: white; color: black; font-family: &quot;Times New Roman&quot;,&quot;serif&quot;; font-size: 18pt; line-height: 115%;"><br /></span><p></p>

 

Friday, September 22, 2023

HAFLA YA BALOZI GASTON KUKABIDHIWA OFISI YA NAIBU MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Dk. Eliezer Mbuki Feleshi akishuhudia makabidhiano ya ofisi kati ya aliyekuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Everisto Longopa (kulia) ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, ya vitendea kazi Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali mpya, Balozi Prof. Kennedy Gaston. Hafla hiyo fupi iliyofanyika katika Makao Makuu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mtumba jijini Dodoma Septemba 20,  2023.Hafla hiyo pia ilihusisha kumuaga Dkt Longopa. 
Balozi Prof. Gaston akikabidhiwa na Jaji Dkt. Longopa nyaraka mbalimbali  za kufanyia kazi.


Jaji Dk. Longopa (kushoto) akimkabidhi rasmi ofisi Balozi Prof. Gaston.
Balozi Prof. Gaston akisaini kwenye kitabu baada ya kukabidhiwa ofisi.
Jaji Dkt. Longopa akizungumza wakati wa hafla hiyo na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Balozi Prof. Gaston.
Balozi Prof. Gaston akitoa neno la shukrani baada ya kukabidhiwa ofisi na Jaji Dkt. Longopa na kuomba ushirikiano na watumishi wa ofisi hiyo.
Katibu Sheria Mkuu wa ofisi hiyo, Esther Cheyo akitoa neno la kumkaribisha Balozi Prof. Gaston.
Mwandishi Mkuu wa Sheria wa ofisi hiyo, Onorius Njole akitoa neno la kumkaribisha Balozi Prof. Gaston kwa niaba ya watumishi wa ofisi hiyo na kuahidi kwamba watumishi wako tayari kutoa ushirikiano kwake.
Baadhi ya watumishi wa ofisi hiyo wakiwa nje tayari kumlaki  Balozi Prof. Gaston.
Balozi Prof. Gaston akikabidhiwa shada la maua alipowasili  katika ofisi hiyo.
Mkurugenzi wa Divisheni ya Uratibu na Huduma za Ushauri wa ofisi hiyo, Dkt. Gift Kweka akitoa neno la kumkaribisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Mhe. Jaji Dkt. Feleshi kuzungumza wakati wa makabidhiano hayo.
Baadhi ya viongozi wa ofisi hiyo.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi akizungumza wakati wa makabidhiano hayo na kuwataka watumishi kutoa ushirikiano wa dhati kwa Balozi Prof. Gaston.


 Mwanasheria Mkuu wa Seikali (AG), Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi (katikati) akiwa na Balozi Prof. Gaston (kulia) pamoja na Jaji Dkt. Longopa.

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA

0754264203


Wednesday, June 22, 2022

Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni, Leo Juni 21,2022 wamejotokeza kuchangia damu na kufanya usafi katika Hospitali ya Uhuru iliyopo katika Wilayani Chamwino mkoani Dodoma.
Watumishi mbalimbali wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,wakichangia damnu katika Benki ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama katika Hospitali ya Uhuru iliyopo Chamwino Mkoani Dodoma ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni. 
Mbali na uchangiaji Damu katika Benki ya damu ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wameshiriki kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Uhuru iliyopo Chamwino Mkoani Dodoma, 
 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni. 
Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakishiriki kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Uhuru iliyopo Chamwino Mkoani Dodoma,  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni. 

Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakishiriki kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Uhuru iliyopo Chamwino Mkoani Dodoma,  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni. 
**********
Na Mwandishi Wetu
KATIKA kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imechangia damu na kufanya usafi katika Hospitali ya Uhuru iliyopo katika wilayani Chamwino mkoani Dodoma.

Watumishi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi wameshiriki utoaji wa damu ikiwa ni kuunga mkono jitihada za kuchangia damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa, akina mama wajawazito na watoto.

Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Chamwino, Dkt. Abdul Pumzi amesema uhitaji wa damu katika hospitali zetu nchini ni mkubwa mno, hivyo amewapongeza watumishi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kujitoa kwao kwa kuchangia damu kama sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma.