KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Thursday, May 30, 2013

MATOKEO MAPYA KIDATO CHA NNE (CSEE) ILIYOFANYIKA OKTOBA 2012.



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI






TAARIFA YA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)  ILIYOFANYIKA OKTOBA 2012


1.0          UTANGULIZI
Mtihani wa Kidato cha Nne, 2012 ulifanyika nchini kote kuanzia tarehe 8/10-25/10/2012. Baraza la Mitihani la Tanzania katika kikao chake cha 94 kilichofanyika tarehe 30 Mei, 2013 liliidhinisha matokeo haya

2.0          USAJILI NA MAHUDHURIO
Jumla ya vituo 5,058 vilitumika katika kufanya mtihani huo ikilinganishwa na vituo 4,795 vilivyotumika mwaka 2011.

2.1          Taarifa za Watahiniwa

Jumla ya watahiniwa 480,029  walisajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wakiwemo wasichana 217,587 sawa na asilimia 45.33 na wavulana 262,442 sawa na asilimia 54.67. Watahiniwa waliofanya mtihani wa Kidato cha Nne 2012  ni 458,139 sawa na asilimia 95.44. Watahiniwa 21,890 sawa na asilimia 4.56 ya watahiniwa wote waliosajiliwa, hawakufanya mtihani.

2.2          Watahiniwa wa Shule
Watahiniwa wa shule waliosajiliwa ni  411,225 wakiwemo wasichana 182,982 sawa na asilimia 44.50 na wavulana 228,243 sawa na asilimia 55.50.  Watahiniwa wa shule waliofanya mtihani walikuwa 397,138 sawa na asilimia 96.57. Aidha, watahiniwa 14,087 sawa na asilimia 3.43 hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo utoro, ugonjwa na vifo.

2.3          Watahiniwa wa Kujitegemea
Watahiniwa wa kujitegemea waliosajiliwa  walikuwa ni 68,804 wakiwemo wasichana 34,605  sawa na asilimia 50.30 na wavulana 34,199 sawa na asilimia 49.70. Watahiniwa 61,001 wakiwemo wasichana 30,918 na wavulana 30,083  wamefanya mtihani wakati watahiniwa 7,803 sawa na asilimia 11.34 hawakufanya mtihani.


3.0          MATOKEO YA MTIHANI

3.1          Maandalizi ya matokeo
Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012 yalitangazwa tarehe 18 Februari 2013 na kufutwa Machi 2013 kutokana na sababu za kitaalamu katika matumizi ya taratibu za kuchakata matokeo. Matokeo yaliyofutwa yalikuwa yamechakatwa kwa kutumia utaratibu wa Fixed Grade Ranges. Matokeo yanayotangazwa sasa yamechakatwa kwa utaratibu huo huo lakini yamefanyiwa Standalization.
Kimataifa kuna aina kuu mbili za kuchakata matokeo ya mtihani : Flexible ‘Grade Ranges na Fixed Grade Ranges’.
‘Flexible Grade Ranges’ hutumia viwango tofauti kuchakata matokeo ya watahiniwa kwa kuzingatia kiwango cha ufaulu cha somo husika kwa kila mwaka. Hivyo viwango vya kuchakata matokeo hubadilika kila mwaka kulingana na ufaulu wa watahiniwa kwa kila somo husika.
Katika mfumo wa ‘Fixed Grade Ranges’ viwango vya aina moja hutumika kuchakata matokeo kwa masomo yote bila kujali kiwango cha kufaulu kwa somo husika. Viwango vya kuchakata matokeo hutumika hivyo hivyo kila mwaka bila mabadiliko.
Kwa miaka mingi Baraza la Mitihani la Tanzania limekuwa likitumia mfumo wa ‘Flexible Grade Ranges’. Mwaka 2012, mfumo wa ‘Fixed Grade Ranges’ ulitumika kuchakata matokeo kwa mara ya kwanza
Mabadiliko hayo yalitokana na maoni ya wadau yaliyotokana na utafiti uliofanywa na Wizara mwaka 2010 kufuatia kushuka kwa ufaulu wa mtihani wa Kidato cha Nne mwaka huo. Pia kwa kuzingatia maelekezo ya Tume maalum iliyochunguza dosari zilizojitokeza kwenye matokeo ya mtihani wa Kidato cha Sita mwaka 2012 katika somo la Islamic Knowledge.

3.2 Matokeo ya Watahiniwa wa Shule
Jumla ya watahiniwa wa shule 159,609 kati ya watahiniwa 397,138
waliofanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wamefaulu. Wasichana walikuwa ni 60,751 na wavulana walikuwa ni 98,858. 


3.3 Matokeo ya Watahiniwa wa Kujitegemea

Idadi ya watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu mtihani ni 26,191 kati ya watahiniwa 61,001 waliofanya mtihani. Wasichana waliofaulu ni 11,581 na wavulana ni 14,910.

4.0          UBORA WA UFAULU KWA MADARAJA NA JINSI

Ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 35,349 wamefaulu katika madaraja I – III ambapo kati yao wasichana ni 10,924 na wavulana ni 24,425.




Mchanganuo wa ufaulu kwa kila daraja kwa jinsi kwa Watahiniwa wa Shule mwaka 2012 ni kama ifuatavyo:


Wavulana
Wasichana
Jumla
Idadi
Asilimia
Idadi
Asilimia
Idadi
Asilimia
I
2,179
1.07
1,063
0.64
3,242
0.88
II
7,267
3.58
3,088
1.85
10,355
2.8
III
14,979
7.37
6,773
4.05
21,752
5.87
I-III
24,425
12.02
10,924
6.54
35,349
9.55
IV
74,433
36.65
49,827
29.78
124,260
33.54
I-IV
98,968
48.66
60,779
36.30
159,747
43.08
0
104,259
51.33
106,587
53.7
210,846
56.92



5.0      SHULE KUMI BORA NA SHULE KUMI ZA MWISHO

Ubora wa shule umepangwa kwa kutumia kigezo cha “Grade Point Average” (GPA) kuanzia A = 1 na F = 5.  Shule zimegawanywa katika makundi mawili kulingana na idadi ya watahiniwa kama ifuatavyo:
(i)            Shule zenye watahiniwa 40 na zaidi  (Jumla ni 3,396)
(ii)           Shule zenye watahiniwa pungufu ya 40 (Jumla ni  753).

5.1     Shule Kumi bora katika kundi la shule zenye watahiniwa 40 na zaidi

Shule zifuatazo zimepangwa kwa kuanza na ya kwanza hadi ya kumi katika kundi la shule zenye watahiniwa 40 na zaidi.


NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI
MKOA
RANK
CENTRE NAME
REGISTERED
REGION
1
ST. FRANCIS GIRLS  S  S
90
MBEYA
2
MARIAN BOYS'  S S
75
PWANI
3
FEZA BOYS' S S
69
DAR ES SALAAM
4
MARIAN GIRLS S  S
88
PWANI
5
CANOSSA S S
66
DAR ES SALAAM
6
FEZA GIRLS' S S
50
DAR ES SALAAM
7
ROSMINI S S
78
TANGA
8
ANWARITE GIRLS  S S
49
KILIMANJARO
9
ST. MARY'S MAZINDE JUU S S
83
TANGA
10
JUDE MOSHONO SS
51
ARUSHA


5.2     Shule Kumi za mwisho zenye watahiniwa 40 na zaidi

Shule zifuatazo zimepangwa kwa kuanza na ya kwanza hadi ya kumi kutoka mwisho.
NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI
MKOA
1
MIBUYUNI  S  S
40
LINDI
2
MAMNDIMKONGO S  S
63
PWANI
3
CHITEKETE  S  S
57
MTWARA
4
KIKALE   S  S
60
PWANI
5
ZIRAI   S S
41
TANGA
6
MATANDA SECONDARY SCHOOL
53
LINDI
7
KWAMNDOLWA   S  S
89
TANGA
8
CHUNO   S.  S
143
MTWARA
9
MBEMBALEO S  S
56
MTWARA
10
MAENDELEO S  S
103
DAR ES SALAAM

5.3          Shule Kumi bora katika kundi la shule zenye watahiniwa chini ya 40

Shule zifuatazo zimepangwa kwa kuanza na ya kwanza hadi ya kumi katika  kundi la shule zenye watahiniwa 40 na zaidi.

NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI
MKOA
1
THOMAS MORE MACHRINA SS  S
20
DAR ES SALAAM
2
QUEEN OF APOSTLES-USHIROMBO SEMINARY
24
SHINYANGA
3
BETHELSABS GIRLS   S  S
33
IRINGA
4
PRECIOUS BLOOD   S  S
34
ARUSHA
5
MAUA SEMINARY
31
KILIMANJARO
6
ST. MARY'S JUNIOR SEMINARY
28
PWANI
7
CARMEL  S    S
36
MOROGORO
8
SANU SEMINARY
37
MANYARA
9
BROOKEBOND  S  S
27
IRINGA
10
ST.CAROLUS SECONDARY   S  S
37
SINGIDA











5.4     Shule kumi (10) za mwisho zenye watahiniwa chini ya 40

Shule zifuatazo zimepangwa kwa kuanza na ya kwanza hadi ya kumi kutoka mwisho.
NAFASI
JINA LA SHULE
IDADI
MKOA
1
DODEANI TECH.    S  S
10
PEMBA
2
KALAMBA    S  S
11
DODOMA
3
HURUI    S   S
12
DODOMA
4
USUNGA    S   S
13
TABORA
5
MANDWANGA    S  S
13
LINDI
6
BETTY MITCHEL  S   S
17
MOROGORO
7
CHONGOLEANI   S  S
17
TANGA
8
MMULUNGA   S   S
17
MTWARA
9
NYUAT    S   S
20
ARUSHA
10
MWAKIJEMBE    S   S
13
TANGA


6.0.      HITIMISHO
Kuanzia sasa matokeo ya mithani ya kidato cha Nne na Sita yatachakatwa kwa kutumia Fixed Grade Range na Standardisation. Natoa wito kwa wadau wote wa elimu kutoa ushirikiano tuweze kuboresha elimu nchini.


7.0.        KUANGALIA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2012

Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE), 2012 yanapatikana katika tuvuti zifuatazo :
·         www.matokeo.necta.go.tz
·         www.necta.go.tz
·         www.udsm.edu.ac.tz, au
·         www.moe.go.tz




Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa (Mb)

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

30/5/2013

No comments: