KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Friday, January 24, 2014

TANGAZO LA KAZI WIZARA YA AFYA NA USTAWI Wa JAMII.



JAMHURI YA MUUNGANO TANZANIA
WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII 

Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii anapenda kuwatangazia nafasi za kazi   kwa wote wenye taaluma  za Kada za Afya ambao wako tayari kufanya kazi katika Utumishi wa Umma.

Vigezo na Masharti:

1.   Awe ni raia wa Tanzania.

2.   Awe na umri usiozidi miaka 45.

3.   Watumishi wa Kada za Afya waliojiendeleza wakiwa kazini wasitume maombi bali waombe kwa Waajiri wao  kubadilishwa vyeo kulingana na sifa walizopata.

4.   Maombi yote yaambatanishwe: Nakala ya Cheti cha Taaluma, Nakala ya Cheti cha Kidato cha Nne/Sita, Maelezo binafsi (CV), Picha (Passport size mbili) za hivi karibuni, Nakala ya cheti cha usajili au leseni ya kufanya kazi ya Taaluma husika.

5.   Vyeti vyote vya Taaluma na Kidato cha Nne/Sita ni lazima vithibitishwe na Hakimu au Wakili  anayetambuliwa na Serikali.

6.   Waombaji wanatakiwa kuchagua/kupendekeza maeneo matatu (Mikoa na Halmashauri)  ambayo wangependa kupangiwa kazi kwa kuzingatia nafasi zilizoainishwa kwenye Kibali (Tazama Tovuti ya Wizara).

7.   Mwombaji yeyote ambaye hatazingatia mojawapo ya masharti au vigezo tajwa hapo juu, maombi yake hayatashughulikiwa.




8. Watumishi ambao walikwishapangiwa vituo vya kazi miaka ya nyuma na
    hawakuripoti au kuacha kazi hawatapangiwa vituo vya kazi, kwa sababu
    hawataweza kuingia kwenye ‘Payroll’ ya Serikali.

Waajiri wote wanatakiwa kuharakisha zoezi la kuwaajiri na kuwaingiza kwenye ‘Payroll’ ya Serikali wataalam wote watakaopangiwa vituo vya kazi kwenye mamlaka zao ikiwa ni pamoja na kuwalipa posho za kujikimu kwa wakati ili kuwaondolea usumbufu usio wa lazima watumishi husika.

 Aidha, Waajiri wanakumbushwa kukagua na kuthibitisha uhalali wa vyeti vya kidato cha Nne na Sita vya wataalam hao kwa kuviwasilisha Baraza la Mitihani la Taifa ili wale watakaobainika kujipatia ajira kwa kutumia vyeti vya kughushi washitakiwe kwa mujibu wa sheria.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, hatatoa barua za kupangiwa Vituo vya kazi.  Majina ya watakaopangiwa vituo vya kazi yatatangazwa kwenye Tovuti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (www.moh.go.tz). Utatakiwa kuripoti kwenye Kituo ulichopangiwa kazi ndani  ya siku 14 kuanzia tarehe ya toleo  la kupangiwa kazi kwenye tovuti ukiwa na vyeti vyako halisi (Original).

Maombi yote yatakayowasilishwa kwa mkono au barua pepe hayatafanyiwa kazi. 
Barua zote zitumwe kwa njia ya posta nafasi inayoombwa  kupitia anuani ifuatayo:-
Katibu Mkuu,
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,
S.L.P. 9083,
DAR ES SALAAM.

Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 7 Februari, 2014.
Tangazo hili pamoja na mchanganuo wa nafasi za kazi  vinapatikana katika tovuti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (www.moh.go.tz)                                                                             

No comments: