KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Wednesday, December 19, 2012

ZUKU NA MAXMALIPO WASAINI MAKUBALIANO NA USHIRIKIANO NA MAXCOM AFRICA LTD KWA WATEJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA MALIPO YA KILA MWEZI KWA WATEJA WAO.

 Meneja  Mkazi wa Zuku Tanzania Ltd,Fadhili Mwasyeba (wa pili kushoto) akizungumza na waandishi (hawapo pichani) Dar es Salaam kuhusu Kampuni ya Maxcom Africa Ltd, ambapo wateja wa Zuku watalipia ada ya kila mwezi kwa kutumia huduma ya Maxmalipo Kushoto ni Meneja Masoko Msaidizi Zuku Tanzania,Veneranda Raphael, Mkuu Uendeshaji Kampuni ya Maxcom Africa Ltd,Ahmed Lussasi (wa pili kulia) na Afisa Mahusiano na Huduma kwa Wateja Maxcom, Maxmalipo Mwanahamisi Hamisi.
Mkuu Uendeshaji Kampuni ya Maxcom Africa Ltd,Ahmed Lussasi (wa pili kulia) akizungumza na waandishi (hawapo pichani) Dar es Salaam kuhusu Kampuni ya Maxcom Africa Ltd, ambapo wateja wa Zuku watalipia ada ya kila mwezi kwa kutumia huduma ya Maxmalipo.Kulia ni Afisa Mahusiano na Huduma kwa Wateja Maxcom, Maxmalipo, Mwanahamisi Hamisi.Wengine ni    Meneja  Mkazi wa Zuku Tanzania Ltd, Fadhili Mwasyeba (wa pili kushoto) na Meneja Masoko Msaidizi Zuku Tanzania,Veneranda Raphael, (PICHA NA TANZANIA LIVE BLOG).


Mkuu wa Uendeshaji Kampuni ya Maxcom Africa Ltd, Ahmed Lussasi,(kulia) akionesha mashine ya Maxmalipo  ya Kampuni hiyo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) Dar es Salaam jana wakati wa kutia saini makubaliano ya Ushirikiano na Kampuni ya Zuku Pay Tv.Wateja wa Zuku watalipia ada zao za mwezi kupitia huduma ya MaxMalipo.Kushoto ni Meneja  Mkazi  Zuku Tanzania Ltd, Fadhili Mwasyeba.(PICHA NA TANZANIA LIVE BLOG).


Dar es Salaam. 
Kampuni ya Zuku Pay TV imetia saini  makubaliano ya ushirikiano  na  Maxcom Africa Ltd ambayo itawezesha wateja  wa Zuku kulipia ada zao wakitumia wakala wa MaxMalipo au mashine  za kulipia za Maxcom. Uzinduzi huu ulifanyika  katika mkutano na waandishi hapa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, Fadhili Mwasyeba  Meneja Mkuu wa Wananchi Satellite Tanzania, wamiliki wa vingamuzi ya Zuku Pay TV,  alisema "Wateja wetu sasa wanaweza kulipia ada za Zuku Pay TV wakitumia technoljia mpya ya MaxMalipo . Zaidi ya hapo wanaweza kupata huduma kutoka mawakala wote wa MaxMalipo kote nchini. Lengo letu kuu ni kutumikia wateja wetu na kuboresha huduma zetu. Makubaliano yetu na MaxMalipo ni ushahidi wa dhamira yetu kuwatumikia wateja wetu.”

Mkuu wa Uendeshaji Kampuni ya Maxcom Africa Ltd, Ahmed Lussasi, alisema "Tunafurahia kuingia makubaliano na kampuni ya Wananchi Sattellite, inayotoa huduma za Zuku Pay TV na kuhudumia wateja wao wote kote nchini. Kampuni yetu inayo mawakala zaidi ya  3500 nchini na huduma yetu mpya ya malipo kwa kutumia mashie maalumu za Maxmalipo inatuwezesha tuwafikie hata wateja katika pembe mbalimbali za nchi. Lengo letu kuu ni kuleta malipo ya elecktroniki karibu na Watanzania. "

Sasa kulipia huduma imerahishwa kwa wateja. Wateja wanatakiwa kuwa na Zuku Subscription ID, kuchagua kati ya huduma ya Zuku Classic, Zuku Premium, Asia Classic au Asia Premium na huduma ya Zuku inawezeshwa papo hapo.

Zaidi ya hapo, Zuku Pay TV sasa wana promosheni ya "Zuku Tunakuthamini - Pata TV Bure". Programu hii ya inayowazawadia wateja, itahitaji wateja wa Zuku kuungananisha wateja  kumi (10) wapya au kuunganisha wateja watano (5) wateja wapyana unashinda televisheni ya inchi 42 na inchi 22. Programu hii hiana draw na ushindi ni wa uhakika.

Televisheni ya Zuku inatoa uchaguzi mpana wa stesheni za burudani ikiwa ni pamoja na Habari, Michezo na Sinema, majarida na muziki. Zaidi ya hapo, wanajumuisha chaneli za nje kama vile BBC, MTV Base, Sentanta Sports, MGM movies na zinginezo nyingi. Pia Msambazaji hutoa ofa kabambe za stesheni kama vile Zuku Afrika ambayo huonesha  bara la Afrika, Zuku Maishaambayo huonesha makala mbalimbali, Zuku Michezo pamoja na chaneli lukuki za sinema. Huduma hii ya Zuku hupatikana kupitia satelaiti Tanzania nzima.

No comments: