Mamlaka
 za Mkoa wa Mwanza zimesema zitatimiza ahadi yao ya kuchangia dola 
118,000 za Marekani (zaidi ya sh. milioni 190) ili kukamilisha mradi wa 
kuweka nyasi bandia kwenye Uwanja wa Nyamagana, jijini Mwanza kabla ya 
Oktoba 15 mwaka huu.
Mkuu
 wa Mkoa (RC) wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo pamoja na Mstahiki 
Meya wa Jiji la Mwanza, Stanslaus Mabula wametoa ahadi hiyo wakati wa 
kikao kati yao na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), 
Leodegar Tenga kilichofanyika leo (Septemba 25 mwaka huu) kwenye ofisi 
za TFF.
Wakuu hao wa Mwanza katika kikao hicho pia walifuatana na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Hida Hassan.
TFF
 ilipeleka mradi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wa 
Goal Project IV wa nyasi bandia wa dola 500,000 za Marekani katika 
Uwanja wa Nyamagana.
Mradi
 huo ulipelekwa huko baada ya Mkoa wa Mwanza kuahidi kuchangia dola 
118,000 ili kukamilisha thamani ya mradi mzima ambayo ni dola 618,000 za
 Marekani. Wamiliki wa uwanja huo ni Jiji la Mwanza.
Goal
 Project I ilitumika kwa ajili ya ujenzi wa hosteli ya TFF (technical 
centre), Goal Project II nyasi bandia Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume 
wakati Goal Project III iliweka nyasi bandia katika Uwanja wa Gombani 
ulioko Pemba, Zanzibar.
Captions:
 Rais wa TFF, Leodegar Tenga (wa pili kushoto) akiwa na ujumbe wa Mkoa 
wa Mwanza ulioongozwa na Mkuu wa Mkoa, Mhandisi Evarist Ndikilo 
ulipomtembelea katika ofisi za TFF jana. Wa tatu kutoka kushoto ni 
Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza, Stanslaus Mabula akifuatiwa na 
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Hida Hassan.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
 
 
No comments:
Post a Comment