KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Monday, January 20, 2014



JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO

Simu ya Upepo       : “N G O M E                      Makao Makuu ya Jeshi,
Simu ya Mdomo    : DSM  22150463                 Sanduku la Posta 9203,
Telex                          : 41051                                   DAR ES SALAAM, 20 Januari, 2014
Tele Fax                     : 2153426
Tovuti             : www.tpdf.mil.tz
                       
Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, kwa mujibu wa Kanuni za Majeshi ya Ulinzi, Aya ya 7.01 Kifungu cha 13 Juzuu ya Kwanza (Utawala), amewapandisha Cheo Maafisa Wakuu kutoka Kanali kuwa Brigedia Jenerali.

Aidha, Maafisa Wakuu hao ni:-
Kanali Denis Raphael Janga, Kanali Jason Nestor Musikula, Kanali Jackson King Mrema, Kanali Martin Amos Kemwaga, Kanali Joseph Cosmas Chengelela, Kanali Martin Nikubuka Mwankanye, Kanali Harold Kidundi Mziray, Kanali Emmanuel Peter Kapesa, Kanali Mwita Wambura Isamulyo, Kanali Francis Asilia Njau, Kanali Pendo Uledi Kamungwele, Kanali Moses Adolph Shinyambala, Kanali Ibrahim Abdarahamani Kimario, Kanali Michael Garo Luwongo, Kanali Nelson Hosea Msanja, Kanali Blasius Kalima Masanja, Kanali Aloyce Damian Mwanjile, Kanali Rajabu Goma Hanti, Kanali Ignas Beatus Mubofu, Kanali Dominic Basil Mrope, Kanali Hamis Issa Majumba, Kanali Salehe Omari Semtaua, Kanali Henry Sweko Kamundo, Kanali Sylivester Msafiri Minja, Kanali John Bangantagoka Bishoge, Kanali Anselm Shigongo Bahati, Kanali Robinson Mboli Mwanjela na Kanali Kaisy Philip Njelekela.


Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Samweli Ndomba kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange amewataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuleta tija na maendeleo katika Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania na Taifa kwa ujumla.

Aidha, Luteni Jenerali Ndomba alisisitiza kusimamia nidhamu na ueledi mambo ambayo ndiyo msingi wa mafanikio katika utendaji wa Majeshi.

Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na  Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P  9203,   Dar es Salaam,  Tanzania.

No comments: