Mke wa Rais
Mama Salma Kikwete akisalimiana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China
Ndugu Li Yuanchao wakati walipokutana kwenye Sherehe ya kutimiza Miaka 50 ya
Uhusiano wa Kidiplomasia baina ya Tanzania na China. Sherehe hizo zilizoandaliwa
na Ubalozi wa Tanzania nchini China na kufanyika jijini Beijing.
Makamu wa Rais wa China Ndugu Li Yuanchao
akigonganisha glasi ikiwa ni ishara ya
kusherehekea kutimiza miaka 50 ya ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania
na China. Sherehe hizo zilifanyika jijini Beijing.
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akigonganisha glasi
na Mke wake Mama Salma wakisherehekea kutimiza miaka 50 ya ushirikiano wa
Kidiplomasia kati ya Tanzania na China.
Rais Dkt.
Jakaya Kikwete na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard Membe wakisherehekea kutimiza miaka 50 ya Ushirikiano wa
Kidiplomasia baina ya Tanzania na Cina kwa kugonganisha glasi zao huku Mama
Salma na Makamu wa Rais wa China Ndugu Li Yuanchao (aliyesimama kulia) wakishuhudia. Sherehe hizo zilifanyika Beijing
nchini China.(PICHA NA JOHN
LUKUWI)
No comments:
Post a Comment