KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Tuesday, March 17, 2015

MAMA SALMA KIKWETE AZURU LINDI/ AHUTUBIA MKUTANO MKUBWA LINDI MANISPAA, AKABIDHI BATI 100 NA VYOMBO VYA BENDI SHULE YA SEKONDARI ANGAZA.

 Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akipokewa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mheshimiwa Mwantumu Mahiza mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Lindi  kuanza ziara ya kikazi ya siku 5 kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM.
 Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mheshimiwa Mwantumu Mahiza akisisitiza jambo wakati akiwahutubia mamia ya wana CCM na wananchi wa Lindi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Mikumbi katika Manispaa ya Lindi.
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea kadi kutoka kwa aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Kata ya Tulieni Mjini Lindi wa Chama Cha Wananchi (CUF) Ndugu Shaibu Rajabu Matola (Kikaptura) aliyeamua kukihama chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi wakati wa mkutano mkubwa uliofanyika kwenye Kata ya Mikumbi.
  Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkabidhi kadi ya CCM Ndugu Shaibu Rajabu Matola mara baada ya kujiunga na chama hicho. Ndugu Matola ni miongoni mwa vijana 200 waliojiunga na Chama Cha Mapinduzi na kukabidhiwa kadi katika mkutano huo.
 Mjumbe wa NEC Taifa ya Chama Cha Mapinduzi na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wananchi wa Manispaa ya Lindi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kata ya Mikumbi.
 Mjumbe wa NEC Taifa ya Chama Cha Mapinduzi na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wananchi wa Manispaa ya Lindi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kata ya Mikumbi.
 Taswira mbalimbali za mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Mikumbi, Manispaa ya Lindi na kuhutubiwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
 Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa Mama Salma Kikwete akikabidhi bati 100 na vifaa vya bendi kwa uongozi wa Shule ya Sekondari Angaza iliyoko katika Manispaa ya Lindi. Anayepokea kwa niaba ya shule hiyo ni Mkuu wa Shule Mwalimu Upendo Muro (wa tano kutoka kulia) akiwa pamoja na Ndugu Ashimun Mzava, Afisa Elimu Sekondar, Manispaa Lindi wa nne kutoka kulia) na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo. Aliyesimama wa kwanza kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilwa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Lindi Bwana Abdallah Ulega.(PICHA NA JOHN  LUKUWI)

No comments: