KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Wednesday, December 14, 2016

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM PAUL MAKONDA ATEKELEZA AHADI ZILIZOTOLEWA WAKATI WA ZIARA YAKE WILAYA TANO ZA MKOA WAKE TOKA TAREHE 19 – 28/11/2016.

 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda akizungumza  kabla ya kutoa ahadi alizoahidi wakati wa zira ya kutembelea Wilaya za Mkoa wake.
 Mkuu wa Mkoa Paul Makonda ,akimkabidhi hundi ya Sh.13,000,000 Meya wa Ilala.
 Akimkabidhi fedha sh.1,000,000,muuza Vitunguu Soko la Temeke Sterio, Evans Mhagama
 Akimkabidhi Sh.200,00 Muuza Supu awali akiuza Machungwa,Zuhura Waziri.
 Waathilika wa Madawa ya Kulevya Sober House wakipokea TV na vifaa vyake.
 Akikabidhi Tumba Afisa habari Makao Makuu ya Jeshi Kombaini ya Bendi,Hope Stanley Dagaa.
 Akimkabidhi Pikipiki Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Buguruni,Baluh Mwakilanga (kushoto) na Mkewe.
 Akizungumza na waandishi wa habari
 Akimkabidhi funguo za gari Kamanda wa FFU Kanda Maalum ya Dar es Salaam,ACP Stanley Kulyamo.
 ACP Stanley Kulyamo. akijaribu gari.
 Akiwakabidhi mabati

 Akimkabidhi Mkuu wa shule ya Katoliki Mifuko 1,000 ya saruji.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam atekeleza ahadi
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul C. Makonda alifanya ziara katika Wilaya zote tano za Mkoa wa Dar es Salaam kuanzia tarehe 19/11/2016 hadi 28/11/2016. Wakati wa ziara hiyo, Mhe. Mkuu wa Mkoa alitoa ahadi mbalimbali kwa jamii, taasisi na watu binafsi. Ahadi hizo zililenga kutoa majawabu kwa kero zilizotolewa na wahusika.
Leo tarehe 14/12/2016 Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam anatimiza ahadi zake kwa kukabidhi vifaa mbalimbali kwa walioahidiwa. Vifaa vinavyokabidhiwa leo vina thamani ya Sh. 164,272,000/=.
Mchanganuo wa ahadi hizo na wahusika ni kama ifuatavyo:
1.     Sober House – kuwaunga mkono juhudi zao za kuwahudumia waathirika wa madawa ya kulevya:
Ø Jiko la Gesi          (540,000/=).
Ø Mitungi 2 ya gesi (240,000/=).
Ø King’amuzi                    (150,000/=).
Ø Television 49’’     (1,750,000/=).
Ø Magodoro 50        (1,250,000/=).
Jumla ndogo       3,930,000/=

2.     Kutokana na utendaji wao uliotukuka Mhe.  Mkuu wa Mkoa ametoa zawadi ya pikipiki ili kuwapa morali ya kazi wafuatao:
Ø Mtendaji wa Kata ya Mbuyuni pikipiki 1 (1,500,000/=).
Ø Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Buguruni pikipiki 1 (1,500,000/=).

Ø Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa zawadi kwa watumishi 4 ambao utendaji kazi wao umedhihirisha hali yao ya utayari wa kujitolea na kufanya kazi kwa ufanisi wa hali yajuu. Watumishi hao wamezawadiwa kulala siku 1 katika Hoteli ya Hyatt the Kilimanjaro kwa gharama ya shilingi 5,232,000/= nao ni:
Ø Dr. Grace Magembe – Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Ø Kamishna Mruto – Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke
Ø Edward Otieno – Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji, Sekretarieti ya Mkoa
Ø Aron Joseph – Mkurugenzi wa Uendeshaji, DAWASCO

3.     Kuunga mkono ujasiriamali:
Ø Kijana wa Soko la Temeke Sterio kupatiwa fedha ili kuimarisha mtaji wake (1,000,000/=).
Ø Mama muuza machungwa amepatiwa kiasi cha shilingi 200,000= ili kuimalisha mtaji wake wa biashara

4.     Kuongeza upatikanaji wa maji:
Ø Kutokana na changamoto ya maji katika Jimbo la Ukonga unaotokana na ubovu wa miundombinu ya kusambazia maji na kufanya kukosekana kwa maji kwa muda mrefu, Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa na kumkabidhi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala cheki ya shilingi 13,000,000/= ili wananchi wa Gongo la Mboto na Pugu waweze kupata maji.
Ø Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa shilingi 500,000/= ikiwa ni mchango kwa ajili ya kukamilisha ununuzi wa tanki la maji kwa wananchi wa Buyuni, Kata ya Pemba Mnazi

5.     Kuunga mkono ujenzi na ukarabati:
Ø Jitegemee Sekondari kupewa mabati 2,000                  (36,000,000/=).
Ø Shule ya Msingi Mbagala Annex kupewa mabati 1,000   (18,000,000/=).
Ø Shule ya Katoliki kupewa mifuko 1,000 ya saruji        (11,000,000/=).
Ø Kutoa matofali 10,000 kwa ajili ya kanisa la AIC (11,000,000/=)
Ø Soko la Samaki Msasani kupewa mabati 300     (5,100,000/=).
Ø Kutoa mabati 200 kwa ajili ya Uwanja wa Taifa (3,600,000/=)

6.     Kuimarisha vikundi vya sanaa (Vifaa vya muziki ):
Ø Kukabidhi Tumba kwa kwaya ya JWTZ            (750,000/=).

7.     Kuimarisha huduma kwa wagonjwa:
Ø Kukabidhi gari la kubeba wagonjwa kwa Polisi FFU Ukonga                                                                                                                    (47,960,000/=)
Ø Kutoa msaada wa fedha za matibabu jumla shilingi 4,000,000/= kwa watu mbalimbali hususan wazee na akina mama.

JUMLA KUU     164,272,000/=

No comments: