![]() |
Taarifa iliyotufikia katika mtandao huu, inaeleza kuwa kuna
ajali imetokea asubuhi leo kuwa katika eneo la Rhotia Wilaya ya Karatu Mkoani
Manyara, iliyohusisha Basi lililokuwa limebeba wanafunzi wa Shule ya
Sekondari ya St Lucky ya jijini Arusha, inayodaiwa kuwa ilipoteza muelekeo
na kupinduka wakati wakiwa safarini kuelekea Karatu waliokuwa wakienda
kufanya mitihani na wanafunzi wenzao wa Shule ya Tumaini English Medium
ya Karatu. Inadaiwa kuwa wanafunzi zaidi ya 20 na walimu wao wamepoteza
maisha huku wengine wakiwa wamejeruhiwa. jitihada za kumtafunda Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Manyara zinaendea ili kupata kauli yake juu ya ajali
hii. Pichani ni baadhi ya wasamalia wakitoa msaada wa uokozi kwa
wanafunzi hao.![]() |
Wasamaria wakitoa miili ya waliokufa.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjl6ft8bMq3KDrdcayz7__xRCAbKbtTAcidn6qkDBkazKCwXW_JyKrHSzDblJiBjcM_YKH1RRQHkS8dfsOSI1nZOk0jJbmeu7yQn56jCWUdjIKbhurJZLr_O15OMn37mLlyE2WG6k0BvqQ/s640/WhatsApp+Image+2017-05-06+at+12.42.59.jpeg)
Uokoaji ukiendelea.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgJEjaH6Yfj7tj9BDZXC3IlBdAIyjviIEHZZ-p0mcY2_M_ltoXiI3_GBdhMdfsieGb_kFnnPQbDZwdVSmIvhF7Qc4UbpLip8cJORnk5uXduyn7gQUnjHSfqAtr-b8JfZM-PFkIfYY4yDQ8/s640/WhatsApp+Image+2017-05-06+at+12.56.06.jpeg)
Gari likiwa katika Bonde.
No comments:
Post a Comment