KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Wednesday, May 27, 2015

VETA YASAINI MAKUBALIANO YA MSAADA NA SERIKALI YA AUSTRALIA .

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA),Mhandisi Zebadiah Moshi akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam.
  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA),Mhandisi Zebadiah Moshi (kushoto) akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam.Wengine Naibu waziri Wizara ya Afya na Utalii wa Australia Magharibi Dk,Kim Hames (wa pili kushoto) Balozi wa Australia nchini John Feakes na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Consolata Mgimba.  
  Naibu waziri Wizara ya Afya na Utalii wa Australia Magharibi Dk,Kim Hames.
 Wageni waliohudhulia  sherehe ya kusaini makubaliano.
 Wageni.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA),Mhandisi Zebadiah Moshi (kulia) na Naibu waziri Wizara ya Afya na Utalii wa Australia Magharibi Dk,Kim Hames (kushoto) wakitia saini makubaliano wakishuhudiwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Consolata Mgimba(kulia) pamoja na Balozi wa Australia nchini John Feakes.
 Wakipongezana baada ya kusaini.
 Wakiwa katika picha ya pamoja viongozi walioshuudiwa kutia saini makubaliano hayo.

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imepata msaada kutoka Serikali ya Australia kupitia Idara ya Biashara na Mambo ya Nje  (DFAT) wa kutengeneza mfumo wa namna ambavyo VETA itakuwa ikishirikiana na viwanda pia waajiri mbalimbali katika kutoa mafunzo ya ufundi stadi. Mfumo huo utakuwa ndio mwongozo wa kuainisha utaratibu wa mafunzo ya ufundi na viwanda au sekta mbalimbali za uchumi mfano sekta ya madini, gesi, utalii n.k.
Mfumo huu utatengenezwa na wataalamu kutoka Australia na Serikali ya Australia imekubali kutoa fedha kiasi cha TSh. 330 milioni kwa ajili ya kazi hiyo.
Manufaa ya mfumo huo kwa VETA itakuwa:-
1)    Kuimarisha mashirikiano na viwanda au waajiri mbalimbali ili kulenga kutoa mafunzo ambayo yanaendana na mahitaji ya soko la ajira.

2)    Utaboresha viwango vya mafunzo yanatolewa na viwanda.

3)    Utapunguza mzigo unaobebwa na Serikali katika kugharamia mafunzo ya ufundi stadi kwa vile viwanda vitakuwa na fursa ya kuchangia gharama za mafunzo kwa njia ya vifaa au kutoa wataalamu wa kufundisha.

4)    Pia walimu wa VETA watakuwa wanajengewa uwezo maana mfumo utawawezesha kufanya mazoezi ya vitendo (practical training) viwandani mara kwa mara ili kunoa ujuzi wao.

5)    Mashirikiano haya yatafungua fursa nyingi za ushirikiano na Taasisi mbalimbali za mafunzo ya ufundi stadi nchini Australia hasa tukizingatia kuwa Australia ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa mafunzo ya ufundi stadi.

Makubaliano ya msaada huo yametiwa saidni leo 27 Mei, 2015 kati ya VETA na Idara ya Biashara na Mambo ya Nje ya Australia katika Hoteli ya Hyatt, jijini Dar es Salaam

Balozi wa Australia Mheshimiwa John Feaks na Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Mhandisi Zebadiah Moshi walisaini makubaliano hayo huku wakishuhudiwa na Naibu Waziri Mkuu wa Jimbo la Australia ya Magharibi, Bw. Kim Hames na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (Tanzania), Bi. Consolata Mgimba.

Balozi wa Australia alisema kuwa, Serikali yake imeamua kuisaidia VETA ili kuimarisha taasisi za elimu na mafunzo ya ufundi na hivyo kuwa na uwezo wa kutoa wahitimu wenye ujuzi wa kutenda kazi katika eneo la gesi, mafuta na madini.

Alisema kuwa msaada huo utalenga zaidi katika kugharimia ushauri wa kitaalam kwenye kuandaa mitaala na kujengea uwezo walimu wa mafunzo ya ufundi stadi.

Australia imefurahi sana kuisaidia VETA katika juhudi zake za kuhakikisha kuwa Watanzania wako katika nafasi nzuri za kutumia na kunufaika na fursa za uwekezaji katika sekta ya madini, gesi na mafuta nchini mwao,” alisema.

Upatikanaji wa wafanyakazi wenye ujuzi wa aina mbalimbali unayapa makampuni makubwa ya uwekezaji fursa ya kuajiri wafanyakazi kutoka ndani ya nchi na hivyo kuwanufaisha wao wenye makampuni na jamii ya ndani, kukuza uchumi wa nchi, hususani kwa kuwapatia wananchi ajira na vipato,” alisema Feakes.

“Tukiwa na uwezo na uzoefu mkubwa katika mafunzo ya ufundi stadi kwenye eneo la mafuta, gesi na madini, tuko radhi kuisaidia Tanzania kunufaika na sekta hiyo,” aliongeza.

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bi. Consolata Mgimba aliishukuru serikali ya Australia na kusema msaada huo utachangia kwa kiasi kikubwa katika kuwawezesha vijana wa Kitanzania kuajirika, utaongeza tija mahali pa kazi na kuchochea ukuaji wa viwanda.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa VETA alisema kuwa pamoja na kupata msaada wa kifedha, VETA inatarajia kunufaika kwa kiasi kikubwa na utaalam na uzoefu kutoka Australia kwa kuwa nchi hiyo ina uzoefu na ujuzi mkubwa kuhusu ushirikiano kati ya taasisi za elimu na mafunzo ya ufundi  kwa upande mmoja na viwanda kwa upande mwingine.

Alisema kuwa ushirikiano huo utasaidia kuboresha mfumo wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini Tanzania.

“Kuwa na mfumo wenye ushirikiano kati ya viwanda na taasisi za mafunzo ya ufundi stadi ni muhimu sana. Ni kupitia mfumo huo ambapo kunakuwa na uhakika wa kutoa rasilimali watu yenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya waajiri, inahakikisha ubora na inawahakikishia wahitimu kuajirika”, Alisema Mhandisi Moshi.

Mfumo huo pia unaweza kuisaidia serikali kupata ahueni ya kugharimia elimu na mafunzo ya ufundi stadi kwa kuwa wenye viwanda wanaweza kuchangia katika utoaji wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi.


Kwa mawasiliano zaidi

Sitta Peter
Meneja Uhusiano
Barua pepe: speter@veta.go.tz
Simu: 0767920019/0652226688

No comments: