KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Friday, September 22, 2023

HAFLA YA BALOZI GASTON KUKABIDHIWA OFISI YA NAIBU MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Dk. Eliezer Mbuki Feleshi akishuhudia makabidhiano ya ofisi kati ya aliyekuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Everisto Longopa (kulia) ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, ya vitendea kazi Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali mpya, Balozi Prof. Kennedy Gaston. Hafla hiyo fupi iliyofanyika katika Makao Makuu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mtumba jijini Dodoma Septemba 20,  2023.Hafla hiyo pia ilihusisha kumuaga Dkt Longopa. 
Balozi Prof. Gaston akikabidhiwa na Jaji Dkt. Longopa nyaraka mbalimbali  za kufanyia kazi.


Jaji Dk. Longopa (kushoto) akimkabidhi rasmi ofisi Balozi Prof. Gaston.
Balozi Prof. Gaston akisaini kwenye kitabu baada ya kukabidhiwa ofisi.
Jaji Dkt. Longopa akizungumza wakati wa hafla hiyo na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Balozi Prof. Gaston.
Balozi Prof. Gaston akitoa neno la shukrani baada ya kukabidhiwa ofisi na Jaji Dkt. Longopa na kuomba ushirikiano na watumishi wa ofisi hiyo.
Katibu Sheria Mkuu wa ofisi hiyo, Esther Cheyo akitoa neno la kumkaribisha Balozi Prof. Gaston.
Mwandishi Mkuu wa Sheria wa ofisi hiyo, Onorius Njole akitoa neno la kumkaribisha Balozi Prof. Gaston kwa niaba ya watumishi wa ofisi hiyo na kuahidi kwamba watumishi wako tayari kutoa ushirikiano kwake.
Baadhi ya watumishi wa ofisi hiyo wakiwa nje tayari kumlaki  Balozi Prof. Gaston.
Balozi Prof. Gaston akikabidhiwa shada la maua alipowasili  katika ofisi hiyo.
Mkurugenzi wa Divisheni ya Uratibu na Huduma za Ushauri wa ofisi hiyo, Dkt. Gift Kweka akitoa neno la kumkaribisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Mhe. Jaji Dkt. Feleshi kuzungumza wakati wa makabidhiano hayo.
Baadhi ya viongozi wa ofisi hiyo.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi akizungumza wakati wa makabidhiano hayo na kuwataka watumishi kutoa ushirikiano wa dhati kwa Balozi Prof. Gaston.


 Mwanasheria Mkuu wa Seikali (AG), Mhe. Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi (katikati) akiwa na Balozi Prof. Gaston (kulia) pamoja na Jaji Dkt. Longopa.

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA

0754264203


No comments: