KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Saturday, December 22, 2012

WAZIRI DK,MUKANGARA ALIPOWATEMBELEA VIJANA NA SACCOS ZILIZONUFAIKA NA FEDHA ZA MKOPO WA MFUKO WA VIJANA MKOA WA MWANZA.

 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  akiongea jambo na Mkurugenzi Msaidizi kutoka  Idara ya Maendeleo Vijana  James Kajugusi  (aliyevaa suti ya blue) jana mara baada ya kumaliza kuwatembelea vijana wajasiriamali wa soko kuu la jijini Mwanza ambao  walipata mkopo kutoka mfuko wa vijana kupitia  Halmashauri ya jiji. Waziri Dk. Mukangara aliwatembelea wajasiliamali hao ili  kuona fedha walizopata zimewasaidiaje  kama kundi la vijana na kijana mmojammoja.
 Mwenyekiti wa SACCOS ya Wafanyabiashara Wadogowadogo Mkoa wa Mwanza (WADOKI)  Mussa Ally akimuonyesha Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  (kulia) mfano wa jengo wanalolitarajia kujenga hivi karibuni kama kitega uchumi chao jijini Mwanza. SACCOS hiyo ilipata mkopo kutoka mfuko wa vijana mwaka 2009 fedha ambazo waliwakopesha vijana wanachama 12.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara  (kushoto) akiongea jambo na  Songaleli Mzee (kulia) ambaye ni mfanyabiashara wa soko kuu la jijini Mwanza aliyepata mkopo kutoka mfuko wa vijana na kufanya biashara ya nafaka. Katikati ni Edward Kabululu  ambaye ni Mwenyekiti wa Mwanza SACCOS ambayo ni moja kati ya 14 za mkoa wa Mwanza zilipata fedha za vijana mwaka 2009 na kumpatia mkopo  Mzee. (Picha na Anna Nkinda – Maelezo)

No comments: