Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Thomas Kashililah
 akitoa ufafanuzi kwa  waandishi wa habari kuhusu ukiukwaji wa kanuni za
 bunge uliofanywa na baadhi ya wabunge wakati wa mkutano wa 10 wa bunge 
uliomalizika mjini Dodoma na mabadiliko yaliyofanyika kwa baadhi ya 
kamati kuondolewa  pamoja na uundwaji wa kamati mpya 3 
zitakazoshughulikia Ushirikiano wa Afrika  Mashariki, Bajeti na Tawala 
za Mikoa na Serikali za Mitaa.
 Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. 
Thomas Kashililah akitoa somo kwa waandishi wa habari kuhusu umuhimu 
wa wabunge kuzisoma na kuzitumia ipasavyo  kanuni za bunge ili kuondoa 
manug'uniko yanayojitokeza pindi wanapozuiliwa na spika kuchangia 
mijadala au kutoa hoja bungeni kwa sababu ya kukiuka kanuni na umuhimu 
wa waandishi wa habari  kuzitumia taarifa rasmi za bunge
katika utoaji wa taarifa zao.
 Waandishi wa habari wakiendelea kupata ufafanuzi wa 
masuala mbalimbali ya uendeshaji wa shughuli za  Bunge kutoka kwa Katibu
 wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah, Dar es salaam. Pamoja na 
mambo mengine amesema ofisi yake itaendelea kushirikiana na vyombo vya 
habari katika utoaji wa taarifa mbalimbali za bunge pamoja na uandaaji 
wa mafunzo ya mara kwa mara kwa waandishi wanaoandika habari za bunge. (Picha na Aron Msigwa - MAELEZO).
 
No comments:
Post a Comment