KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Monday, September 2, 2013

LAW Africa YATOA MSAADA WA VITABU VYA SHERIA KWA VYUO VIKUU MBALIMBALI NCHINI.



Taarifa hii yahusu zoezi la utoaji vitabu vya sheria kwa vyuo vikuu mbalimbali vinavyofundisha masomo ya sheria hapa nchini.  Kampuni ya LawAfrica  ambayo inafanya shughuli za kibiashara za uchapishaji na usambazaji wa vitabu vya sheria katika nchi za Africa mashariki imeamua kutoa msaada wa vitabu mbalimbali vya sheria katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu ili kuweza kuchangia juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali na wadau wengine katika kuboresha taaluma hii muhimu hapa nchini. Malengo mengine ya zoezi hili ambalo litakuwa endelevu ni kama yafuatayo:
1.     Kuhamasisha wachapishaji wengine kutoa misaada ya vitabu katika sekta ya elimu na katika ngazi tofauti yaani katika ngazi ya shule za msingi, sekondari na vyuo vikuu

2.     Kuhamasisha wadau wengine kuchangia sekta ya elimu kwa kutoa misaada ya vitabu ambavyo ndio vitendea kazi vikuu kwa walimu katika kufundisha  na wanafunzi pia katika kujifunza.

3.     Kutoa changamoto kwa wanafunzi na pia kwa watanzania wote kiujumla kujenga mazoea ya kujisomea vitabu. Tabia ya kujisomea vitabu na machapisho mbalimbali hutuwezesha kuwa na uelewa mpana katika maswala mbalimbali  yanayoizunguka jamii yetu na ulimwengu kiujumla.

4.     Kuhamasisha waandishi wa Kitanzania hasa katika taaluma ya sheria  kwani tuna waandishi wachache sana ambao wameandika vitabu ukilinganisha na nchi jirani kama vile Kenya na Uganda. LawAfrica inawakaribisha wale wote wenye nia ya kufanya hivyo kwani kampuni yetu iko tayari kuchapisha vitabu katika Nyanja ya sheria pasipo mwandishi kuchangia gharama yoyote.
Kwa awamu hii ya kwanza jumla ya vyuo kumi na nne (14) kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania vimeweza kunufaika na msaada huu wa vitabu.
Ni malengo ya kampuni ya LawAfrica  kulifanya zoezi hili kuwa endelevu ili kuweze kufikia vyuo vyote hapa nchini na pia zoezi hili linafanyika pia katika nchi ya Uganda na Kenya.


TAARIFA HII IMETOLEWA NA:

GWAKISA GEORGE MAKARANGA
MENEJA MKUU WA LAWAFRICA TANZANIA
+255 782 00 44 22

Meneja Mkuu wa Law Africa Tanzania, Gwakisa Makaranga (wa tatu kulia) akimkabidhi mmoja wa wawakilishi wa Vyuo Vikuu sehemu ya Vitabu vya Sheria, Mkuu wa Idara ya Sheria Muhadhiri na Mkuu wa Mahakama ya mfano Chuo Kikuu cha Dodoma,Njiti Batthy,(kushoto) makabidhiano hayo yalifanyika jana Dar es Salaam,Wengine kutoka kushoto ni Martin Massawe (Chuo kikuu cha Mzumbe),Rehema Kaunda,(Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam) Anthony Mwenda (Tumaini Dar es Salaam) Josephine Lawi (Chuo cha Teofilo Dar es Salaam) na Tumainiel  Lyimo wa Chuo cha Sebastian kolowa Memorial Lushoto.

No comments: