KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Thursday, August 14, 2014

Jwtz Kufanya Uzinduzi wa Tiba ya Bure Kwa Wananchi.



JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
KURUGENZI YA HABARI NA MAHUSIANO

Simu ya Upepo   : “N G O M E            Makao Makuu ya Jeshi,
Simu ya Mdomo : DSM  22150463      Sanduku la Posta 9203,
Telex                     : 41051                         DAR ES SALAAM, 14 Agosti, 2014
Tele Fax                : 2153426
Barua pepe       : ulinzimagazine@yahoo.co.uk
Tovuti                  : www.tpdf.mil.tz

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), linatarajia kuzindua huduma ya Tiba kwa jamii kuanzia   tarehe 15 Agosti  2014 hadi 19  Agosti 2014 kuanzia saa 12:00 asubuhi hadi 12:00 jioni katika viwanja vya Mnazi mmoja.  Huduma hizi zinakwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 50 ya JWTZ.
Huduma zitakazotolewa ni pamoja na vipimo vya magonjwa ya Homa ya Ini (Hepatitis B& C), Presha, Kisukari, Huduma za Ushauri nasaha na kupima VVU, Huduma za uchangia damu salama, Macho, Kinywa na Koo.  Kwa vipimo vya Malaria, matibabu yatatolewa hapo hapo.   Huduma zote hizo ni bure.
Nafasi hii itatoa mwanga wa kuweza kuona ueledi wa madakitari wetu wazalendo ambao ni matunda yenu.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo anatarajiwa kuwa Waziri wa Afya Dk Selemani Seif Rashidi.   JWTZ linawakaribisha wananchi wote.
          Aidha tunakialika chombo chako cha habari kuhudhuria kufanya  coverage’ ya tukio hilo.
          Tumelinda, tunalinda, tutalinda daima Taifa letu Tanzania.

Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na  Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203,   Dar es Salaam,  Tanzania.
Kwa Mawasiliano zaidi: 0754 - 270136

No comments: