KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Wednesday, December 7, 2016

WAAMUZI WAONDOLEWA RATIBA YA LIGI KUU YA VODACOM.

Waamuzi waliochezesha mchezo namba 49 kati ya Yanga na Simba, Martin Saanya na Samweli Mpenzu wametolewa kwenye ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, huku suala lao likipelekwa kwenye Kamati ya Waamuzi ili ishughulikie tatizo lao kitaalam.
Maamuzi hayo yamefanyika baada ya Kikao cha Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji ya Bodi ya ligi, kuwaita na kuwahoji na kuangalia mkanda wa mchezo husika. Kamati imebaini mapungufu mengi ya kiutendaji yaliyofanywa na waamuzi hao, na hivyo kuitaka kamati ya waamuzi ishughulikie.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

KATIBU WA RHINO AFUNGIWA KWA KUIDANGANYA KAMATI YA SAA 72

Kamati ya usimamizi na uendeshaji imempa adhabu ya Kumfungiwa miezi mitatu Katibu Mkuu wa Rhino Rangers, Dickson Cyprian Mgalike kwa kosa la kuidanganya kamati kwa kutoa taarifa potofu katika barua aliyoiandikia Bodi ya Ligi.
Hapo awali, Kamati ilimuadhibu Mchezaji Sameer Mwinyishere kwa kosa la kumrushia chupa ya maji mwamuzi.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

ZIARA YA TIMU YA TAIFA MPIRA WA MIGUU U15
Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya Vijana wa Tanzania wenye umri wa chini ya miaka 15, kesho Desemba 8, 2016 inaanza rasmi ziara ya mkoani Morogoro ambako watakuwa na mchezo wa kirafiki kesho jioni na keshokutwa asubuhi.
Vijana hao 22, walioko kambini kujiandaa Dar es Salaam wanajiandaa na mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Shelisheli unaotarajiwa kufanyika Desemba 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

No comments: