KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Monday, May 6, 2013

MAMA SALMA KIKWETE ZIARANI NCHINI KUWAIT.

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akifurahia kazi za mikono zinazofanywa na watoto wenye ugonjwa wa akili (autism) wakati alipotembelea Kuwait Autism Center huko nchini Kuwait. Mama Salma amefuatana na Rais Kikwete katika ziara ya siku tatu ya kiserikali nchini humo.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiangalia kazi za useremala zinazofanywa na watu wenye ugonjwa wa akili wa watoto (autism)  wakati alipotembelea Kuwait Autism center. Mama Salma yupo nchini Kuwait akifuatana na Rais Kikwete kwenye ziara ya kiserikali ya siku tatu nchini humo.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, akifurahia jambo na Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Kuwait Center for Autism Dr. Samira Al Saad mara baada ya bkusaini kitabu cha wageni baada ya kuwasiri kituoni hapo.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, akifurahia jambo na Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Kuwait Center for Autism Dr. Samira Al Saad mara baada ya bkusaini kitabu cha wageni baada ya kuwasiri kituoni hapo.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiaagana na Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Kuwait Autism Center Dr. Samira Al Saad mara baada ya kutembelea taasisi hiyo iliyopo nchini Kuwait.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikaribishwa na Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Kharafi Kids Activity Center Bibi Sabeeka Al Jaser wakati Mama Salma alipotembelea kituo hicho kilichoko katika jiji la Kuwait  kinachotunza watoto na watu wenye matatizo mbalimbali kama vile wenye mtindio wa ubongo.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiangalia kazi za uchoraji zinazofanywa na watu wenye ulemavu wa ubongo wanaolelewa katika kituo Kharafi Kids Activity Center wakati Mama Salma alipotembelea kituoni hapo
Mama Salma Kikwete akiangalia ufinyanzi wa vitu mbalimbali unaofanywa na watu wenye ulemavu kwenye Kituo cha Kharafi huko nchini Kuwait.
Baadhi ya watoto wenye ulemavu wa akili wanaolelewa katika kituo cha Kharafi Kids Activity Center kilichoko huko Kuwait wakishiriki katika ufumaji wa nguo na vitambaa mbalimbali kama anavyoshuhudia Mama Salma Kikwete alipotembela kituoni.
Baadhi ya watoto wenye ulemavu wa akili wanaolelewa katika kituo cha Kharafi Kids Activity Center kilichoko huko Kuwait wakishiriki katika ufumaji wa nguo na vitambaa mbalimbali kama anavyoshuhudia Mama Salma Kikwete alipotembela kituoni.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wafanyakazi wa Kharafi Kids Activity Center baada yan kutembelea kituo hicho kilichoko katika jiji la Kuwait.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiagana rasmi na Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Kharafi Kids Activity Center Bibi Sabeeka Al Jaser mara baada ya kutembelea kituo hicho kilichoko Kuwait City
(PICHA NA JOHN LUKUWI)

No comments: