Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya
Rufaa, Semistocles Kaijage (wa tatu kutoka kushoto) na Makamu Mwenyekiti wa
Tume Jaji Mst. Zanzibar, Hamid M. Hamid (wa tatu kutoka kulia) wakiwa katika
picha ya pamoja na watendaji wa NEC walipotembelea vituo vya kupigia kura
katika Jimbo la Dimani kuangalia maandalizi ya Uchaguzi mdogo wa Ubunge
utakaofanyika Jumapili, Januari 22, 2017.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya
Rufaa, Semistocles Kaijage (kulia) akiangalia Orodha ya majina ya wapiga
kura 603 iliyobandikwa katika kituo cha kupigia Kura cha Skuli ya Maandalizi ya
Nyamanzi katika jimbo la Dimani Zanzibar. Wengine ni Mkurugenzi wa Huduma
za Sheria wa NEC, Emmanuel Kawishe (katikati) na Msimamizi Msaidizi wa
Uchaguzi wa Jimbo la Dimani, Idaya Seleman Hamza.
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa NEC, Emmanuel Kawishe
(katikati) akimweleza jambo Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji
(R), Semistocles Kaijage (kushoto) alipotembelea kituo cha kupigia kura cha
Skuli ya Maandalizi ya Nyamanzi katika jimbo la Dimani. Kulia Msimamizi
Msaidizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Dimani, Idaya Seleman Hamza.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya
Rufaa, Semistocles Kaijage (kulia) akiangalia Orodha ya majina ya wapiga
kura 603 iliyobandikwa katika kituo cha kupigia Kura cha Skuli ya Maandalizi ya
Nyamanzi katika jimbo la Dimani Zanzibar. Kulia ni Msimamizi Msaidizi wa
Uchaguzi wa Jimbo la Dimani, Idaya Seleman Hamza.
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mst.
Zanzibar, Hamid M. Hamid (katikati) akifafanua jambo kwa Mwenyekiti wa
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R). Semistocles Kaijage (kushoto) na
Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa NEC, Emmanuel Kawishe mara baada ya
kutembelea kituo cha kupigia kura cha Dimani visiwani Zanzibar.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji wa Mahakama ya
Rufaa, Semistocles Kaijage (kushoto) akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa Tume Jaji Mstaafu wa Zanzibar, Hamid M.Hamid (wa pili kutoka kushoto) na Watendaji wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi mara baada ya kutembelea vituo vya kupigia kura katika jimbo la
Dimani. Katikati ni Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa jimbo la Dimani, Idaya
Selemani Hamza, Mkurugenzi wa huduma za kisheria, Emmanuel
Kawishe (wa pili kutoka Kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Daftari la Kudumu la Mpiga Kura Mhandisi Isack Manyiri.
No comments:
Post a Comment