![]() |
Meneja Matekelezo Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, WCF, Victor Luvena, (kulia), akiwahudumia waajiri waliofika kujisajili na kulipa michango.![]() |
|
NA
K-VIS BLOG/Khalfan Said
MUITIKIO
wa waajiri kujisajili na kulipa michango katika Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi
(WCF) umekuwa wa kuridhisha hususani Mwezi Agosti, Meneja Matekelezo Victor
Luvena amesema.
Itakumbukwa ya kwamba, tarehe 23 Julai 2017 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama (Mb), alitoa siku 30 kwa waajiri wote nchini ambao walikuwa hawajasajili kuhakikisha wanajisajili katika Mfuko na wanawasilisha michango kwa wakati, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao na kama Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi inavyoelekeza.
“Kwakweli
tunamshukuru Mheshimiwa Waziri kwa agizo alilolitoa kwani limetoa msukumo mkubwa,
waajiri wengi wamejitokeza kutekeleza wajibu wao wa kisheria wa kujisajili na
kuwasilisha michango katika Mfuko.” Alisema Luvena
K-VIS Blog ilishuhudia idadi kubwa ya waajiri wakiwa wamejitokeza ambayo ndiyo siku ya mwisho kwa waajiri kutekeleza agizo la
Mheshimiwa waziri, wakiwa wamejazana kwenye ofisi za WCF kujisajili na kuwasilisha michango, ambapo
kazi hiyo ya kuwahudumia ilikuwa ikiongozwa na Meneja Matekelezo - WCF, Victor Ruvena.
|
Waajiri, wakihudumiwa na maafisa wa WCF.
Afisa Matekelezo wa WCF, Gladness Madembwe, (kulia), akimkabidhi cheti cha usajili,Sultani Ali kutoka kampuni ya Marifas Refregerator ya jijini Dar es Salaam.
Afisa Matekelezo wa WCF, Edward Kerenge, (kushoto), akiwahudumia waajiri waliofika kujisajili na Mfuko.
Afisa Matekelezo wa WCF, Edward Kerenge, (kulia), akiwahudumia waajiri waliofika kujisajili na Mfuko.
Afisa Matekelezo Msaidizi wa WCF, Emiliana J.Gwagilo, akimsikiliza Mwajiri huyu aliyefika kupatiwa huduma.
Afisa Matekelezo Msaidizi wa WCF, Emiliana J.Gwagilo, (kushoto), akimuhudumia Mwajiri huyu aliyefika kupatiwa huduma.
Afisa Matekelezo wa WCF, Gladness Madembwe,(kushoto), akimuhudumia Bw. Sultani Ali kutoka kampuni ya Marifas Refrigeration, ya jijini Dar es Salaam.
Meneja Matekelezo Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, WCF, Victor Luvena, (kulia), akiwasikiliza waajiri waliofika ili kupatiwa huduma ya usajili na uwasilishaji michango katika Mfuko huo.
Maafisa wa WCF (kulia), wakimsikiliza Mama huyu mwajiri aliyefika kupatiwa huduma.















No comments:
Post a Comment