KWA MAWASILIANO ZAIDI: E-mail: yusuf.badi2@gmail.com.

NSSF

TANGAZO

Tuesday, September 26, 2017

WAKURUGENZI MKOANI SINGIDA WAAGIZWA KUNUA CHAKI ZINAZOZALISHWA MKOANI HUMO.


Mkuu wa Mkoa wa Singida,Dk Rehema Nchimbi akishiriki kazi ya uzalishaji chaki wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea Kiwanda cha usagaji wa unga wa Gypsum na Uzalishaji chaki cha Dober Color Kilichopo katika Kata ya Itigi-Majengo Halmashauri ya Itigi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida,Dk Rehema Nchimbi akikagua kiwanda cha usagaji wa unga wa Gypsum na Uzalishaji chaki cha Dober Color Kilichopo katika Kata ya Itigi-Majengo Halmashauri ya Itigi wakati wa ziara ya kikazi
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi,Miraji Jumanne Mtaturu akimkabidhi boksi tano za chaki Mkuu wa Mkoa wa Singida,Rehema Nchimbi mara baada ya kutembelea na kukagua kiwanda cha usagaji wa unga wa Gypsum na Uzalishaji chaki cha Dober Color Kilichopo katika Kata ya Itigi-Majengo Halmashauri ya Itigi wakati wa ziara ya kikazi
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Miraji Jumanne Mtaturu akishiriki kazi ya uzalishaji chaki wakati wa ziara ya kikazi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida,Dk Rehema Nchimbi kutembelea Kiwanda cha usagaji wa unga wa Gypsum na Uzalishaji chaki cha Dober Color Kilichopo katika Kata ya Itigi-Majengo Halmashauri ya Itigi.

    Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Rehema Nchimbi akisalimiana na Meneja wa kiwanda cha Uzalishaji chaki cha Dober Color, Mukhtar Mahamood mara baada ya kuwasili kiwandani hapo

Mkuu wa Mkoa wa Singida,Dk Rehema Nchimbi akikagua mizinga ya nyuki mara baada ya kutembele kiwanda Uzalishaji chaki, Mafuta ya Alizeti na Asali cha Fahari Kilichopo katika eneo la Tambukareli Halmashauri ya Mji wa Itigi wakati wa ziara ya kikazi, Kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu.

Ukaguzi wa kiwanda cha uzalishaji Chaki

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Rehema Nchimbi akikagua eneo la kutunzia Unga wa Gypusm katika kiwanda cha uzalishaji Gypsum cha Sanjaranda, Halmashauri ya Itigi

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Rehema Nchimbi akizungumza kwa njia ya simu na mmiliki wa kiwanda cha uzalishaji unga wa Gypsum cha Sanjaranda Bw Rashid Said Rashid akiwa Dar es salaam ambaye alimuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa mpaka kufikia Januari 2018 uzalishaji wa Gypsum utaanza katika eneo la Sanjaranda, Halmashauri ya Itigi ili kurahisisha huduma hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida,Dk Rehema Nchimbi akiwa kwenye shamba la Mkulima Juma Patrick na kujionea mikorosho inavyoharibika kwa kukosa dawa ambapo alizungumza kwa njia ya simu na muwakilishi wa Bodi ya Korosho akiwa Dar es salaam ambaye alimuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa dawa za kuua wadudu kwenye Mikorosho zitawasili kati ya Jumanne  Septemba.
Mkuu wa Mkoa wa Singida,Dk Rehema Nchimbi akionyesha chaki bora zinazozalishwa Wilayani Manyoni Mkoani Singida.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Rehema Nchimbi akisalimiana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Itigi,Ally Minja mara baada ya kuwasili Kwa ajili ya kutembelea Kiwanda vya usagaji unga wa Gypsum na uzalishaji chaki.
Miongoni wafanyakazi wa kiwanda cha  Uzalishaji chaki cha Dober Color wakiendelea na kazi wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Rehema Nchimbi.

No comments: